728x90 AdSpace


Monday, June 27, 2016

MJUE ALIYEMTOA KIJASHO DIAMOND PLATNUMZ 'BET'

Japo kiunaga ubaga, mjue mshindi wa tuzo za BET katika 'kategori' ambayo Diamond Platnumz alibahatika kuwa mmoja kati ya waliochaguliwa kuwania. 

Ilikuwa ni tuzo ya msanii bora kutoka Afrika, ambapo katika kategori hiyo ilikuwa na wasanii wafuatao:

1.WIZKID (NIGERIA)


2. AKA (SOUTH AFRICA)

 

3. SERGE BEYNAUD (COTE D’IVOIRE)

 

4. CASSPER NYOVEST (SOUTH AFRICA)

 

5. MZVEE (GHANA)

 

6. YEMI ALADE (NIGERIA)

 

7. DIAMOND PLATNUMZ (TANZANIA)

 

8. BLACK COFFEE (SOUTH AFRICA)......MSHINDI

 

 Jina lake halisi ni Nkosinathi Innocent Maphumulo, jina lake la kisanaa/kimuziki anaitwa Black Coffee/ Dj Black Coffee, alizaliwa tar. 11March 1976 (miaka 40) huko Durban, Afrika kusini. 
Black Coffee ni muandaaji wa muziki (record producer), DJ, mwimbaji/msanii pia mjasiriamali. Alianza kuonekana sana kwenye tasnia ya muziki mnamo mwaka 1995 na anafanya vizuri mpaka leo.

Mwaka 2011, Black alifanikiwa kufunga ndoa na muigizaji na mwongozaji wa filamu Bi. Mbali Mlotshwa, familia ya Coffee imebahatika kuwa na watoto wanne, ambapo wawili ni watoto wa mke wake wa sasa (Mbali Mlotshwa) na wawili ni wa mahusiano yaliyopita ya star huyo (Black).

 Mpaka sasa Coffee ametoa albamu 5 ambazo ni Black Coffee (2005), Have Another One (2007), Home brewed (2009), Africa Rising (2012) na Pieces of Me (2015).


Zifuatazo ni tuzo ambazo Black Coffee amewahi kupata.



2005: SAMA Best Urban Dance Album
2010: South African Music Awards#12th South African Music Awards .282006.29
2010: SAMA Best Male Artist
2010: Health Magazine Best Man
2010: Metro FM Award for Best Produced Album
2010: Metro FM Award for Best Dance Album
2011: Channel O Award for Most Talented Male Artist
2012: Sunday Times Generation NEXT Award for Coolest DJ
2013: SAMA Best Dance Album
2013: Sunday Times Generation NEXT Award For Coolest DJ 2013
2014: Sunday Times Generation Next Award for Coolest DJ
2015: DJ Awards for Breakthrough DJ Of The Year
2016: SAMA Best Dance Album
BET Award for Best International Act: Africa





Tunaamini katika kila shindano kama hili lazima apatikane mshindi mmoja na haimaanishi walioshindwa hawajui au hawafai, ni wakali ila inatakiwa apatikane mkali mmoja hivyo Hongera sana kwa wote waliokuwa 'Nominated' kwenye kategori hiyo. Hongera sana kwa Diamond platnumz kwa kuwa mmoja wapo na kuiwakilisha Tanzania katika tuzo hizo. Hongera nyingi kwa Black Coffee kuwa mshindi katika kategori hiyo na kuwa msanii wa kwanza kutoka Afrika Kusini kupata tuzo ya BET.

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: MJUE ALIYEMTOA KIJASHO DIAMOND PLATNUMZ 'BET' Description: Rating: 5 Reviewed By: Eddy